Wednesday, 20 August 2014

Marekani yalaani mauaji ya mwandishi

James Foley
Rais Barack Obama wa Marekani amesema mauaji ya mwandishi wa habari James Foley raia wa Marekani aliyeuawa na wapiganaji wa kundi la Kiislam yameishtua dunia.
Obama amesema kitendo hicho ni cha kikatili na kisichokubalika mbele za Mungu na kwamba ni matokeo ya mawazo duni yasiyoendana na karne ya sasa.
Kauli hiyo ya Rais Obama inakuja huku wazazi wa mwandishi huyo wakielezea kutoridhishwa kwao na hatua zinazochukuliwa na Marekani kutokana na mauaji ya mtoto wao.
Wazazi hao wamesema wakati mwingine waandishi wa habari huru hawathaminiwi katika aki zao hata pale wanapojitolea maisha yao kwa ujira mdogo

0 comments:

Post a Comment

 

Subscribe to our Newsletter

Contact our Support

Email us: youremail@gmail.com

Our Team Memebers