Tuesday, 19 August 2014

Dudu Baya: Sijabahatika kumpata mwanamke ninayemtaka, nakutana na machizi

 Msanii wa Hip Hop kutokea Mwanza, Godfrey Tumaini aka Dudu Baya amesema kuwa majanga anayopata kwenye mahusiano yake yanatokana na kutompata mwanamke anayemhitaji.

 Akizungumza na Mkasi TV hivi karibuni, Dudu Baya amesema wanawake wengi anaokutana naowanakuwa ni machizi. “Kwanza sijabahatika kukutana na mwanake ambae mimi namtaka, nafikiri Mungu bado hajanipa huwaga nakutana na machizi, kwa sababu mimi sipendi, mwanamke aliyelelewa na kufundwa vizuri vitu vya ndani huwezi ukavitoa nje. 

Msanii DUDU BAYA
 Kwa mimi binafsi siongeagi  kwa wanaume wengine, napenda sana siri za familia zibaki kuwa siri za familia. Kwa mfano huyu jinsi alivyoenda kwenye media asitarajie nimtamrudia kabisa, ile tabia ya kwenda kwa jirani na kanga moja ikianguka? Kweli kabisa kicheni party zinaendelea lakini hazisaidii kitu chochote,” alisema

0 comments:

Post a Comment

 

Subscribe to our Newsletter

Contact our Support

Email us: youremail@gmail.com

Our Team Memebers